04/05/2026
JINI HALIWEZI KUKUTII NA KUKUFANYIA KAZI YAKO KABLA YA WEWE HUJALITII HILO JINI KATIKA HAJA ZAKE
Na wanaeleza Wanawachuoni ikiwemo sheikhul Islam Ibnu Taymiyah Rehemahullaah kwamba Miongoni mwa masharti ambayo Jinni anampa mwanaadamu ili amfanyie kazi yake ni pamoja na kuinajisi Qur-aan (kuitilia haja ndogo, au kubwa au hedhi au nifasi Quran au kuichana) au kufanya jambo la uovu sana ambalo litamkasirisha Allah Subhaanahu Wata'ala, mfano kumuingilia kimwili mama yako mzazi n.k.
Kwahiyo ukifanya jambo hilo atalokuamrisha ndipo nayeye atakutekelezea hilo ulitakalo k**a ni kukupa pesa, mali, cheo, umaarufu n.k
Na hakika Uislamu umepiga vita mambo haya kwani ni ushirikina.
Allaah Subhaanahu wata aalaa Anasema
إِنَّهُۥ مَن يُشۡرِكۡ بِٱللَّهِ فَقَدۡ حَرَّمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ ٱلۡجَنَّةَ وَمَأۡوَىٰهُ ٱلنَّارُۖ وَمَا لِلظَّٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٖ
"Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Janna / Pepo, na makazi yake yatakuwa ni motoni Na madhalimu hawatopata yeyote mwenye kunusuru.
Suratul Al-Maaida Aaya 72.
"Uchawi ni makubaliano baina ya mchawi na Jinni akishurutishwa mchawi kufanya mambo ya haramu au ya shirki, na baada ya kufanya hayo, Jinni anashurutishwa kumsaidia na kumtii mchawi huyo kila anachotaka".
Baadhi ya yale ambayo mchawi anatakiwa na Sheitani ayatende ili ajikurubishe naye ni:
1 - Mchawi anatakiwa auvae msahafu miguuni na aingie nao chooni
2 - Aandike baadhi ya aya za Qur-aan kwa damu ya hedhi
3 - Miongoni mwao wanashurutishwa kuandika aaya za Qur-aan penye nyayo za miguu
4 - Au aiandike Suuratul-Faatiha kinyume nyume
5 - Aswali bila ya Wudhuu
6 - Wengine hutakiwa kuchinja mnyama bila ya kulitaja jina la Allaah kisha amtupe mnyama huyo mahali maalum anapoamrishwa na Sheitani
7 - Wamo miongoni mwao wanaozungumza na nyota au kuzisujudia
8 - Au hutakiwa kuandika herizi kwa maneno yenye kufru ndani yake
Imeelezwa kwamba katika nchi ya Shaam / Syria kulikuwa na mtu ambaye watu walikuwa wakimpenda na kumheshimu sana wa