Aviation Tanzania

Aviation Tanzania A digital media platform delivering trusted insights, perspectives, and stories on the development of the aviation industry locally and globally.
(1)

https://whatsapp.com/channel/0029VaG0R8tAe5VzPI8VZL2k
Connecting Aviation Stories, People & Progress

11/08/2026

Mwezi uliopita,Julai 2026 macho ya dunia yalikuwa nchini Uturuki, kwenye mkutano wa viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya kujihami ya mataifa ya magharibi (NATO). Miongoni mwao aliohudhuria mkutano huo ni Rais wa Marekani Donald Trump, ambaye baada ya mkutano huo alitarajiwa kurejea nyumbani k**a kawaida. Lakini safari yake ya kurejea Marekani haikuwa ya kawaida kabisa.

Kwa mujibu wa taarifa ya The Washington Post, hofu ya uwezekano wa Iran kumlenga Trump wakati wa safari yake ya kurejea Marekani ilikuwa kubwa kiasi kwamba, licha ya kufika Uturuki kwa kutumia ndege mpya iliyotolewa na falme ya Qatar, Rais huyo hakurejea moja kwa moja Marekani akiwa ndani ya ndege hiyo.

Badala yake, maafisa wa usalama waliamua kutumia ndege ya zamani ya Air Force One, yenye rangi ya bluu na nyeupe, kusafirisha wafanyakazi wa Ikulu na waandishi wa habari. Hatua ambayo ilionekana kuwa sehemu ya mpango wa kiusalama ambao haukujulikana kwa watu wengi waliokuwa ndani ya ndege.

Video iliyorekodiwa siku hiyo inaonyesha Trump akipanda ngazi za Air Force One na kuwaaga watu waliokuwa uwanjani. Lakini muda mfupi baadaye, takribani dakika tano, waandishi wa habari walipanda ndege hiyo huku lori la huduma za chakula likiondoka eneo hilo.

Lori hilo lilionekana baadaye likielekea nyuma ya ndege nyingine ya kijeshi iliyokuwa imeegeshwa karibu na Air Force One. Na Taarifa zinaeleza kuwa Trump alikuwa ndani ya lori hilo la chakula na baadaye alihamishiwa kwenye ndege hiyo ndogo ya kijeshi, ambayo ilikuwa karibu na Air Force One.

Hatua hiyo ya kumhamisha Rais kwa siri inadaiwa kufanywa kwa lengo la kufanya safari yake isiwe rahisi , huku Air Force One ikiwa tayari inajulikana na kufuatiliwa kwa urahisi zaidi.

Taarifa hiyo inakuja wakati ambapo serikali ya Marekani imekuwa ikisisitiza kuwa kuna maadui wengi wa Marekani wanaomlenga Rais Trump, na kwamba vyombo vya usalama hutumia kila njia iliyopo kukabiliana na vitisho hivyo.

11/08/2026

Mwanamke mmoja kutoka nchini uingereza anayefahamika k**a Betty Bromage, amevunja rekodi ya dunia kwa kuwa mwanamke mwenye umri mkubwa zaidi kutembea kwenye mabawa ya ndege ikiwa angani.

Betty mwenye umri wa miaka 97 alivunja rekodi ya dunia ya Guinness (Guinness World Record) Agosti 4,2026 , baada ya kusimama juu ya bawa la ndege ndogo ambayo ilifanya safari ya dakika tano.

Mwanamama huyo amefanya tukio k**a hilo mara sita katika maisha yake, na safari yake ya kwanza aliifanya mwaka 2016 alipokuwa na umri wa miaka 87.

Alipozungumza na vyombo vya habari, Betty alisema aliamua kufanya hivyo tena kwa sababu hataki kuchoshwa na maisha, licha ya kutoweza kuendesha gari na kuwa na changamoto ya kuona vizuri.

Safari hiyo pia ililenga kuchangisha fedha kwa ajili ya hospitali ya Cheltenham General, ambayo ilimpatia matibabu baada ya kupata kiharusi mwezi Agosti 2025.

Bromage alisema hospitali hiyo ilimhudumia vizuri, huku akieleza kuwa kiharusi hicho kiliathiri maisha yake, lakini kwa ujumla anaendelea vizuri.

10/08/2026

Ethiopia has inaugurated a new passenger terminal at Dejazmach Belay Zeleke International Airport in Bahir Dar, making it the country’s largest airport terminal outside Addis Ababa Bole International Airport.

The terminal was officially inaugurated on August 6, 2026, by Prime Minister Abiy Ahmed as part of efforts to improve transport infrastructure and support Bahir Dar’s growing economic and tourism activities.

The upgraded facility is expected to improve passenger handling and ease congestion as demand for air travel between Bahir Dar and Addis Ababa continues to grow.

Bahir Dar is a major tourism gateway to Lake Tana, the Blue Nile Falls and historic monasteries, making the airport an important part of the city’s tourism and economic development.

🇪🇹

Coastal Air is inviting qualified candidates to apply for an Avionics Engineer position.Applicants should have full expe...
10/08/2026

Coastal Air is inviting qualified candidates to apply for an Avionics Engineer position.

Applicants should have full expertise in aircraft avionics systems and a minimum of five (5) years’ relevant experience. Experience with Cessna Caravan and Pilatus PC-12 aircraft is an added advantage. Tanzanian nationals are preferred.

Applications should be submitted via email to [email protected]

Application deadline: 21st August 2026.

10/08/2026

Mwalimu wa marubani mwenye umri wa miaka 21, anayejulikana k**a Emily Shelton, amelazimika kutua kwa dharura kwenye barabara kuu ya magari iliyopo katika mji wa Pensacola, Florida nchini Marekani baada ya ndege aliyokuwa akiirusha aina ya Piper PA-28 Cherokee kupata hitilafu ya injini wakati wa safari ya mafunzo ya urubani.

Tukio hilo lilitokea wakati Emily Shelton alipokuwa akimfundisha Rubani mwanafunzi ambaye alikuwa kwenye safari yake kwanza ya vitendo.

Wakiwa angani, huku ndege hiyo ikiendeshwa na Rubani mwanafunzi, Shelton aligundua harufu ya mafuta ndani ya chumba cha marubani, huku shinikizo la mafuta kwenye injini likianza kushuka kwa kasi.

Baada ya kugundua kuwa wasingeweza kurejea kwenye uwanja wa ndege, alichukua udhibiti wa ndege hiyo kutoka kwa mwanafunzi wake kisha kuwasiliana na waongozaji wa safari za ndege na kuwajulisha kuwa watalazimika kutua kwenye barabara kuu ya Interstate 10.

Kwa kutumia ujuzi wake wa urubani, alifanikiwa kuielekeza ndege hiyo chini ya bango kubwa lililokuwa juu ya barabara na kutua salama katikati ya magari yaliyokuwa yakipita.

Licha ya kutua katika eneo lenye magari yanayotembea, Shelton, mwanafunzi wake na watu waliokuwa chini hawakupata majeraha.

Shelton ana takribani saa 1,300 za uzoefu wa kurusha ndege, na amesema alikuwa amewahi kufanya mazoezi ya namna ya kukabiliana na hali ya dharura k**a hiyo. Hata hivyo, hakutarajia siku moja angelazimika kutumia mafunzo hayo katika tukio halisi.

Uchunguzi wa awali umebaini kuwa ndege hiyo ilitua kwa dharura kutokana na tatizo la shinikizo la mafuta ya injini (oil pressure)

Kwa sasa, Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Marekani (FAA) inaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha hitilafu hiyo ya injini.

Skyward Airlines Limited, the General Sales Agent (GSA) for South African Airways in Kenya, is hiring for several positi...
09/08/2026

Skyward Airlines Limited, the General Sales Agent (GSA) for South African Airways in Kenya, is hiring for several positions:

- Sales Executive – Nairobi
- Customer Service Agent – Reservations – Town Office
- Customer Service Agent – Airport Operations & Ticketing – JKIA
- Customer Service Agent – Check-in – Migori & JKIA

Interested and qualified candidates can apply via www.skywardairlines.com/careers

📅 Application Deadline: Friday, 14 August 2026

Only shortlisted candidates will be contacted. Skyward Airlines Limited is an equal opportunity employer committed to merit-based recruitment.

08/08/2026

Abiria wawili nchini Urusi, wamedhibitiwa na polisi baada ya kuingia katika eneo la maegesho ya ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sheremetyevo, baada ya kuchelewa kufika uwanjani hapo kwa ajili ya safari yao ya ndege.

Abiria hao waliingia kwenye eneo la apron wakijaribu kuifikia ndege ya shirika la Aeroflot, ambayo tayari ilikuwa ikivutwa na gari maalumu tayari kwa kuanza safari.

Wafanyakazi wa uwanja wa ndege pamoja na polisi waliingilia kati, kuwaondoa abiria hao katika eneo hilo na kuwazuia kupanda ndege.

Aviation Tanzania Network wishes everyone a happy Nane Nane Day.
08/08/2026

Aviation Tanzania Network wishes everyone a happy Nane Nane Day.

Kampuni ya Swissport Tanzania, kwa kushirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania Tanzania Airports Authority ime...
07/08/2026

Kampuni ya Swissport Tanzania, kwa kushirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania Tanzania Airports Authority imezindua rasmi ghala la kisasa la kuhifadhi bidhaa zinazohitaji halijoto maalum katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro.

Ghala hilo linatarajiwa kuimarisha uwezo wa Tanzania katika usafirishaji wa mizigo kwa njia ya anga, hususan bidhaa zinazohitaji kuhifadhiwa katika halijoto maalum k**a vile maua, matunda, mboga na bidhaa nyingine zinazouzwa katika masoko ya kimataifa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw.Abdul Mombokaleo, alisema viwanja vya ndege vina mchango mkubwa katika kukuza uchumi kwa kuunganisha wazalishaji, wafanyabiashara na masoko ya kimataifa.

Aliongeza kuwa TAA itaendelea kuboresha miundombinu ya viwanja vya ndege na kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ili kuongeza ufanisi wa huduma, biashara na maendeleo ya uchumi wa taifa.

07/08/2026

Ukifika katika makao makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania Tanzania Civil Aviation Authority moja ya vitu vinavyoweza kukuvutia ni uwepo wa ndege iliyowekwa k**a kumbukumbu mbele ya jengo hilo.

Ndege hiyo ilipata usajili wake kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania tarehe 20 Juni 1995, ikiwa na namba ya usajili 5H-SJS.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Aviation Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Aviation Tanzania:

Shortcuts

Share